REPOSITORY

UCHANGANUZI WA KIISIMU WA UHALIFU KATIKA MITANDAO YA FACEBOOK NA BARUAPEPE

Show simple item record

dc.contributor.author MWANGI, JAMES
dc.date.accessioned 2025-04-08T08:46:37Z
dc.date.available 2025-04-08T08:46:37Z
dc.date.issued 2024-07-01
dc.identifier.uri http://repository.laikipia.ac.ke/handle/123456789/3582
dc.description.abstract Mawasiliano yameimarika sana katika karne ya ishirini na moja kufuatia uvumbuzi wa teknolojia ya habari na matumizi ya intaneti. Kuimarika kwa hali ya kutangamana kwa watu kwenye mitandao kumeongeza visa vya uhalifu. Mawasiliano ya mitandaoni yamesababisha kuwepo kwa diskosi nyingi za mitandaoni ambazo ni tofauti na diskosi za maandishi na za mazungumzo ya moja kwa moja. Uhalifu wa mitandaoni ni uovu ambao umekuwepo kutoka wakati ambao uvumbuzi wa intaneti ulipotokea. Wahalifu wa mitandaoni hutumia baruapepe, Instagram, Twitter, Facebook, To-go WhatsApp na njia nyingine nyingi za mitandao kuwadanganya na kuwaibia watu hela. Lugha hutumika katika mitandao hii kuwashawishi watumiaji ili kuingia katika mitego yao miovu. Wahalifu hutuma jumbe za ushindi wa pesa, ugawaji urithi, jumbe za kibiashara, udukizi, uduhushi na utoaji wa pesa na ulaghai wa ushindi katika michezo ya kamari. Utafiti huu ulichunguza aina mbalimbali za uhalifu katika mitandao ya Facebook na baruapepe, kuchanganua mikakati ya ushawishi inayotumiwa na wahalifu na kuhakiki mbinu za lugha katika jumbe za kihalifu katika mitandao hii miwili. Nadharia ya Uchanganuzi wa Mawasiliano ya Kiupatanishi ya Kitarakilishi ya Herring pamoja na nadharia ya Ushawishi iliyoasisiwa na Aristotle kisha kuendelezwa na Hovland na Cialdini zilitumika. Utafiti huu ulifanyika maktabani huku ukihusisha ukusanyaji wa data kwa njia ya kupakua jumbe pamoja na picha katika mitandao ya Facebook na baruapepe. Mbinu ya kiuthamano ilitumiwa katika uchanganuzi wa data. Muundo wa utafiti ulikuwa wa kimaelezo kwa kutoa ufafanuzi wa mambo yote kwa kina katika kila hatua. Sampuli ya utafiti iliteuliwa na mtafiti kimakusudi kwa kutumia jumbe na picha mia moja ambazo baadaye zilichujwa hadi arubaini na saba mintaarafu ya madhumuni ya utafiti. Data iliyokusanywa ilionyesha kuwa mikakati ya ushawishi kama vile imani na maadili, utoaji wa hoja zenye mantiki na hisia hutumiwa sana kushawishi watumiaji wa mitandao hii hadi kufikia kiwango cha kuwatapeli watumiaji. Vilevile, ilibainika kuwa wahalifu wa mitandaoni hutumia mbinu nyingiza lugha kama vile takriri, mdokezo, mbinu rejeshi, nidaa, imoji, simulizi, maswali ya balagha na nyinginezo ikiwa ni njia moja ya kufaulisha mazungumzo yao na kushawishi watumiaji wa mitandao. Utafiti pia ulibainisha kuwepo kwa aina mbalimbali za uhalifu kwenye mitandao hii kama vile utapeli, uumbuaji, unyanyasaji wa kimapenzi, vitisho, ubaguzi na propaganda za kiuchochezi. Utafiti huu utawafaa wasomi na watafiti wa lugha kwa sababu, utawezesha watafiti wengine kuwa na ari ya kuchambua diskosi na kauli tofauti tofauti kama zinavyotumiwa na watu katika mitandao na kuweza kupambanua maana kwenye muktadha. Zaidi ni kuwa matokeo yake yataongeza maarifa kwa watafiti kwa kuchambua namna nadharia ya Mawasiliano ya Kiupatanishi ya Kitarakilishi na ya ushawishi zinaweza kutumiwa kubainisha mitindo mbalimbali ya matumizi ya lugha na mikakati ya mawasiliano ambayo huonyesha dalili za uhalifu wa mitandaoni na jinsi ufahamu huu unaweza kutumiwa kama mikakati ya kujizuia na kupunguza uhalifu wa mitandaoni. en_US
dc.language.iso en en_US
dc.publisher LU en_US
dc.subject UCHANGANUZI WA KIISIMU WA UHALIFU KATIKA MITANDAO en_US
dc.subject UHALIFU KATIKA MITANDAO YA FACEBOOK NA BARUAPEPE en_US
dc.subject JAMES MWANGI en_US
dc.title UCHANGANUZI WA KIISIMU WA UHALIFU KATIKA MITANDAO YA FACEBOOK NA BARUAPEPE en_US
dc.type Thesis en_US


Files in this item

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search DSpace


Browse

My Account